Waandishi wetu
KUMEKUCHA! Nyota
wa sinema za Kibongo, Jimmy Mafufu ameibuka na kuwa msanii wa kwanza
kutangaza nia ya kugombea ubunge wa Jimbo la Mbeya Mjini kwa ‘leseni’ ya
Chama Cha Mapinduzi (CCM).
Akipiga
stori na safu hii juzi jijini Dar, Mafufu alisema amefikia uamuzi huo
baada ya kuombwa na wananchi wa jimbo hilo kwa vile mbunge wa sasa,
Mheshimiwa Joseph Mbilinyi ‘Sugu’ kupitia Chama cha Demokrasia na
Maendeleo (Chadema) hajatimiza ahadi zake.
“Nakwenda
Mbeya, Ijumaa (Leo) nitatua kwenye Uwanja wa Ndege wa Songwe,
nitapokelewa pale na wana-CCM tayari kwa kuanza mchakato wa kuchukua
fomu kwa tiketi ya CCM kugombea ubunge. Ni mimi tu ndiye nitakayeiweza
Mbeya Mjini,” alisema Mafufu.
CHANZO EDDY BLOG