Ripoti ya jana Alhamis ilionyesha idadi ya watu 96 kupoteza maisha kutokana na ajali ya moto iliyotokea katika kituo cha mafuta katika mji mkuu wa Accra Ghana.
Baadhi ya magari yaliyokuwa katika kituo hicho yakiwa yameungua kabisa
Hii ni idadi ya vifo ambayo imeonyesha kuongeza ambapo mpaka sasa watu waliofariki wamefikia 175 kutokana na ajali hiyo.
Moto huo uliozuka siku ya jumatano usiku wakati wakazi wa mji huo walipokuwaeneo hilo wakijikinga na mvua kubwa ambayo imewaacha raia wengi bila makaazi pamoja na kukosekana kwa umeme kwa muda mrefu.
Lori ambalo limebeba miili ya watu waliokufa kwenye moto huo likichuruzisha damu
Serikali ya Ghana imetangaza siku tatu za maombolezo ya kitaifa kufuatia vifo hivyo.
Mmoja wa majeruhi akisimulia ajali hiyo



