Pazia la shindano la kuimba Bongo Star Search mwaka 2015, limeanza rasmi leo mkoani Mwanza ambapo usaili umefanyika kwenye hoteli inayojulikana kama Lakairo.
Shindano hilo linaloibua vipaji vya vijana mwaka huu lina kauli mbiu
mpya ya ‘Kuwa Original Chagua Original’ ambayo inawahimiza vijana
kujitokeza na kuonesha vipaji vyao.
Shindano hilo la kusaka vipaji vya kuimba kwa mwaka linatafanya usaili
mikoa 4 ambapo Mwanza July 4-5 ndani ya ukumbi wa La kairo, July 11-12
Arusha ukumbi wa Triple 7, Mbeya ukumbi wa Club vibes July 18-19 na Dar
July 24-26.