ISABELA ANASWA NA MCHEPUKO AKIDENDEKA DAKIKA CHACHE KABLA YA KUVISHWA PETE

AMA kweli duniani kuna mambo! Mdada anayehangaika kutafuta jina katika tasnia ya muziki wa Kibongo, Isabella Mpanda ‘Bella’ aliitia doa sherehe yake ya kuvishwa pete ya uchumba baada ya kunaswa akidendeka na mchepuko dakika chache kabla ya tukio hilo muhimu.

Mbongo Fleva Masoud Karama ‘Luteni Kalama’ akimvisha pete mpenzi wake wa kitambo, Isabella Mpanda ‘Bella’.

Msanii huyo alivishwa pete na mpenzi wake wa kitambo, Mbongo Fleva Masoud Karama ‘Luteni Kalama’, wiki iliyopita ndani ya Ukumbi wa Kakala uliopo Kigamboni, Dar lakini dakika 20 kabla ya tukio hilo alinaswa katika kona moja ya ukumbi huo akidendeka na mchepuko ambaye pia ni Mbongo Fleva, Inspector Haroun.

Paparazi wetu ambaye alikuwepo ukumbini hapo aliwanasa wawili hao katika kona moja yenye giza wakiwa ‘mahaba niu’e huku Inspector akionekana kuwa na wasiwasi wa kuonwa na mwenye mali.

Baada ya kushtushwa na mwanga wa kamera, wawili hao walionekana kuweweseka kwanza kisha, Inspector akaanza kumwomba paparazi wetu kuzifuta picha hizo akidai zikionekana zinaweza kumletea matatizo.

“Kaka soo bwana… soo kaka! Huyu ni shemeji yangu, hapa tuna hang’ tu… noma mkubwa. Hizo picha zikionwa nitafikiriwa vibaya na ‘mwanangu’ (Kalama),” alisema Inspector kwa sauti ya unyenyekevu. Bella yeye alisema: “Halafu hawa kwa kufuatafuata watu hawajambo. Futa bwana hizo picha.”

wdcfawqafwef